Site icon Al Kags

kiswahili cha tukuzwa kweli?

Nimekua nikiwaza kwamba hii lugha yetu pengine imedidimia kiasi kwamba hakuna atakae ijibu blogi hii. Aghalabu ni kwamba kiswahili sanifu hakizungumzwi tena humu nchini na hata nadra zaidi huko ulaya.

Nivipi hivi sisi wana-nyayo tumekipuuza kiswahili kama ambae hatukukisoma? Katika kazi yangu nimeona biashara kadhaa ambazo nina maono kwamba ni biashara za kesho. Kunazo zile za kusukumiza kazi, yaani outsourcing. Ukiwatafuta warembo wakuzungumza kimombo kutokea puani wapo wengi humu nchini na bila shaka biashara yako ya kusukumiza itafana hasaa ikiwa ni ya simu kutoka marekani na uingereza.

kiswahili twakiweza tena au tumekitupa?

nakumbuka nikiwa mchanga kulikua na wimbo kwenye runinga, ulioanzisha kipindi fulani cha watoto wa shule za msingi. wimbo wenyewe ulikua “kiswahili kitukuzwe, kwani lugha ya taifa…”

je, tufutilie mbali lugha hii au tuijenge?

Exit mobile version